Kampuni ya PAN Africa Power Sulition (PAP), wamefungua kesi Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, asubuhi hii, kuomba mahakama itoe amri ya zuio la muda la kuzuia bunge kujadili wizi wa fedha kwenye akaunti ya Escrow.

Kesi hiyo ni Misc Civil Application Na. 50 ya 2014 ambayo ni kesi ya msingi na maombi ya zuio ni Misc Civil Application 51 2014 a- Injunction - ambako pamoja na mengine, mahakama imeobwa kutoa amri ya kulizuia bunge kujadili Escrow akaunti.

Washitakiwa katika kesi hii, ni Spika wa Bunge, Katibu wa Bunge, CAG, TAKUKURU na katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini. Kumekucha!